Umekwisha wahi kuona? Mtu anag’ang’ana kufukazana na
vijimambo vidogo vidogo tu mtaani wala hakuna kinachoeleweka. Ndio! watu hao
wapo wengi tu, wao ni wachambuzi wa kila
neno litokalo vinywani mwa wengine.
Ni wataalamu waliobobea kuhakikisha
hawakosi sifa mtaani, kijiweni, ofisini, shuleni, chuoni, gengeni na kila
sehemu walipo. Ingekuwa heri kama sifa hizo ni za mambo mema , rakini mara
nyingi ni yale yasiyofaa hata kutamkwa. Wanaweka sifa pasipohitaji sifa.
Ukitambua
Chagua Njia Yako
Nataka nikuhimize uchague njia yako mwenyewe ya maisha,
jiamulie wewe mwenyewe njia utakayopitia.
Usiige mtu fanya kile ukipendacho.
Nikijichukulia kwa mfano mimi, kufundisha ni kitu ninachokipenda sana. Sipendi
kuajiriwa kama mwalimu wa shule lakini napenda
kufundisha kwa namna yoyote ile. Najisikia raha sana ninavyoandika makala hizi za kuwahamasisha watu wachukue hatua kuelekea mafanikio yao. Hii ni njia niliyoichagua mimi.
kufundisha kwa namna yoyote ile. Najisikia raha sana ninavyoandika makala hizi za kuwahamasisha watu wachukue hatua kuelekea mafanikio yao. Hii ni njia niliyoichagua mimi.
Usijaribu kuniiga
ikiwa siyo njia yako vinginevyo iwe ni moja ya njia ulizokuwa umezichagua
kufuata.
Kichwa
Cha Habari
Wafalme
Hupigana Kwa Ajili Ya Himaya, Vichaa Hupigana Kwa Ajili Ya Sifa. hayo
ni maneno ya mwandishi mashuhuri wa mashairi kutoka Uingereza anaitwa John
Dryden. Anatupatia picha halisi ya kile kinachoendelea katika jamii yetu.
Nimekutana na baadhi ya watu ambao kutokana na fursa walizozipata, huwezi
kumwambia chochote. Utakuta mtu sio kwamba hapambani bali anapambana sana kwa ajili ya maisha yake
yamkini na kwaajili ya maisha ya watu wengine wanaomzunguka.
Tatizo ni njia ipi
anayotumia kupambana huko?. Zamani ilionekana ukiwa mwalimu kila mtu mjini na
kijijini atakusalimia kwa heshima “shikamoo mwalimu”; lakini siku hizi ukiwa
mwalimu unaogopa hata kusema kama wewe ni mwalimu. Unafikiri ni kwanini?
Sio
kwa sababu ualimu hauna heshima wala sio kwa sababu kuwa mwalimu sio njia
sahihi ya kupambana! Hapana bali kinachotokea akilini mwa watu wengi kulingana
na maendeleo ya teknolojia na ukuaji wa uchumi na kuongezeka kwa fursa duniani,
watu wengi wameanza kubadili mawazo yao na kuanza kuona kwamba kuajiriwa ni
njia mojawapo ya kuanzia maisha nasio njia ya kukufanya uwe tajiri.
Ninachotaka kusema ni kwamba, kuajiriwa tu halafu
ukabaki unajisifia kwamba wewe ni mtumishi wa Serikali na unacheo kikubwa na
kwahiyo yoyote na yeyote anayekushauri wa chini yako unaona kama anakushauri
upuuzi na unapotezea halafu unakomaa kusubiri “Pension yako” na unajiona uko
sahihi kabisa, hiyo ndiyo aliyoisema John Dryden kwamba “Wafalme Hupigana Kwa
Ajili Ya Himaya, Vichaa Hupigana Kwa Ajili Ya Sifa”.
Unahitaji
Neno Moja Tu
Imewahi kutokea kwako?
Siku moja ukaamka unahuzuni moyoni na hupati
picha jinsi utakavyo vuka changamoto za maisha zinazokukabili. Ukafanya kila
njia ya kukufariji na kukufanya upate ahueni lakini hukupata ahueni hata
kidogo.
Ukawasha mziki wa kila aina uupendao lakini mziki unaonekana kama mziki
wa “waswezi”(hawa ni watu wanaofanya sherehe za matambiko huko Unyamwezini na
usukumani),yaani kwa kifupi mziki haupandi.
Je haijahi tokea wakati ukiwa
katikati ya mawazo magumu namna ile halafu ukasikia sauti au neno moja au ukasoma sehemu halafu gafla kila kitu
kimefunguka, furaha inarudi unapata nguvu japo shida iliyokuwa inakusumbua bado
haijaisha? Je, hali hiyo haijawahi kutokea kwako? Kwanini ulipata furaha
katikati ya shida nyingi zikiwa bado zinakukabili?
Kwanini
Unaenda Kusali?
Sijui kwa upande wako lakini mimi imetokea mara nyingi
kama sio kila siku, nikienda Kanisani kusali kuna neno moja hunigusa kuliko
maneno mengine na kunifanya nifikiri upya juu ya msimamo wangu wa maisha. Kuna
maneno mengi sana huzungumzwa Kanisani au Msikitini lakini katika yote hayo neno moja tu
ndilo litakalokugusa na kukufanya uanze kuishi maisha mapya ndani ya nuru
uliyoipata kwenye ibada. Kama unafikiri nasema uongo nisamehe bure.
Kwanini usingekuwa unabaki nyumbani tu ukachukua kitabu
chako cha dini ukajisomea?. Jibu ni rahisi sana kitu kipya husisimua ubongo
wako na kuongeza umakini. Unahitaji mtu mwingine aseme kwa ajili yako ili
kuamsha akili na ari ndani yako. Ukitaka kuwa kichaa kama alivyosema bwana John
Dryden funga mlango wako wa ndani wa kusikia. Maneno yote mzuri yatakuja lakini
yatakuta mlango umefungwa hayataingia moyoni mwako na matokeo yake utakuwa
unajiona uko vizuri kumbe ni kichaa.
Tunafahamu Unajua Mambo Mengi Lakini….
Hatutaacha kusema na wewe na wala hatutaacha
kukuandikia makala au hatuaacha kuwasiliana na wewe kwa njia yoyote ile.
Kwanini tuwasiliane na wewe mara kwa mara kwa njia ya makala, semina, simu au
hata ana kwa ana?
JIBU: Tunafahamu kwamba unahitaji neno moja tu ili
likutie nguvu kuelekea mafanikio yako. Maadamu umeamua kufikia mafanikio
makubwa ya kiuchumi neno letu moja
litakusaidia sana. Tunafahamu kunachangamoto nyingi za kimaisha, huenda kuna kitu kimekutoa kwenye mstari wa
kuelekea mafanikio makubwa, kwa kupitia makala zetu huenda kuna neno litakugusa
na kufungua upya nia ya kusonga mbele kuelekea mafanikio yako.
Usiache kusoma makala hata kama ina kichwa cha habari
kisichobeba mvuto kwako mimi nakushauri jilazimishe uisome makala yote huenda
kuna neno moja au ushauri utakugusa sana halafu utapata wazo jipya au mbinu
mpya ya kusonga mbele. “We need to be
rich”
Glasi
Iliyojaa Maji Inahitaji Kuongezwa Ukubwa Ili Ibebe Maji Mengi
Kwa kujifunza kutoka kwa watu mbalimbali hasa
waliofanikiwa duniani nimepata kuelewa kwamba, unaweza kujiona uko vizuri kumbe
wewe ni glasi iliyojaa maji. Hata tone moja likiongezwa kwenye glasi hiyo, matone mwili au matatu yatamwagika chini.
Maana yake kuna mahali akili zetu na mioyo yetu inakuwa glasi iliyojaa maji.
Hata aje mtu wa aina gani akwambie kuna fursa nzuri ya kufanya wala hushituki
wala hakuna hamu ya kumsikiliza wala hujali kabisa, wakati maisha magumu yanakugonga. Hii ni
dalili kwamba wewe ni glasi iliyojaa maji. Huhitaji kujua jambo jipya
umeridhika na mbinu unazotumia au unazofikiria huhitaji kujua mbinu nyingine.
Mimi nasema kufanikiwa kwako kutakuwa kwa shida sana.
Baada ya kugundua kwamba kumbe mtu anaweza kuwa glasi
iliyojaa maji, mimi nilikataa katu katu, kwamba sitaki kuwa glasi iliyojaa maji. Kwa
sababu hiyo nikaifundisha akili na moyo wangu lazima utengeneze glasi kubwa
ambayo haitajaa maji. Ndivyo nilivyo mpaka sasa, kwangu kujifunza sifikirii kama nitamaliza
kesho au mwaka kesho au miaka kumi ijayo sifikirii hivyo hata kidogo, kujifunza
kwangu ni siku zote na wakati wote maadamu niko hai.
Kwa kujizoeza hivyo akili na moyo wangu siku zote usiku na mchana unahamu ya kujua mambo ambayo siyajui. Nikisikia kesho kuna semina ya ujasiriamali moyo unatamani na akili inakusanya akili zake ili iweze kusikia kwa makini na kuengeneza taswirw ya kile ninachokisikia pia inaandaa umakini wa kusikiliza maana nahitaji neno moja tu nisonge mbele.
Sijafika mbali lakini kasi ni nzuri sana, imani yangu siku moja nitafika mbali. Sijaamua kusafiri pekee yangu tu kuelekea mafanikio makubwa nataka kwenda na kila mtu aliye na mzigo ndani yake wa kufikia mafanikio makubwa. Ndio maana nakutumia makala hizi ili tusonge mbele.
Kanuni Ya 20% Kwa 80%
Hii ni kanuni ya ulimwenguni kote kwamba 20% wa watu
katika idadi ya watu fulani ni matajiri na 80% ya watu katika idadi hiyo hiyo
ya watu ni maskini. Wewe ungependa kubaki kwenye 80%? Kama unabaki huko endelea
kubaki mimi nimeshagoma. Ukiweza na wewe kugoma, goma na weka msimamo wa
kuhamia kwenye 20%. Imetosha kwa leo.
0 comments:
Chapisha Maoni