Hii ni aina mojawapo ya kiasili
kilichoundwa kwa protini na mafuta (yaani glycoprotein) ambacho
kinapatikana juu ya uso wa seli nyeupe za damu zijulikanazo kama Thelper
Cells, Regulatory T-Cells, Monocytes, Macrophages na Dendritic Cells
ambazo kazi yake kubwa ni kupambana na maradhi mbalimbali.
Zimepewa jina la CD4 kuonesha kuwa ni
aina ya nne katika kundi la viasili vya CD. Kazi zake kubwa ni kusaidia
baadhi ya chembe nyeupe za damu kupambana na wadudu waenezao maradhi
mbambali katika mwili wa binadamu.
CD4 husaidia kukuza na kupitisha taarifa
kutoka kwenye vipokeo vilivyopo kwenye T-Cells. Taarifa hii
huzitahadharisha chembechembe nyeupe za damu kujiandaa kupambana na
vidudu vilivyovamia mwili kwa kutumia njia mbalimbali. Aina hii ya
chembechembe nyeupe za damu inayopambana na uvamizi wa mwili huitwa
T-Lymphocytes.
CD4 ni aina ya protini inayopatikana
katika ukuta wa seli zinazojulikana kama T-Helper Cells (pia hujulikana
kama CD + Lymphocyte).
Virusi vya Ukimwi (VVU) hushambulia na kujishikiza kwenye protini hii kabla ya kupata uwezo wa kuathiri seli za T-Helper.
Seli hizi za T-Helper ndizo hulinda mwili dhidi ya maambukizi mbalimbali na hivyo kuchangia katika kustawi kwa kinga ya mwili.
Kupungua kwa seli hizi mwilini husababisha kupungua kwa kinga ya mwili na hivyo mtu kupata magonjwa nyemelezi.
Kupungua kwa seli hizi mwilini husababisha kupungua kwa kinga ya mwili na hivyo mtu kupata magonjwa nyemelezi.
Baadhi ya magonjwa nyemelezi yanayoweza kumpata mtu mwenye ugonjwa (VVU/Ukimwi) ni pamoja na magonjwa ya mfumo wa kupumua kama vile ugonjwa wa Homa ya Mapafu (Pneumocyctic Carinii Pneumonia), Kifua Kikuu (TB) na Saratani.
Mengine ni magonjwa ya mfumo wa chakula kama vile Cryptosporidiosis, Candida (fangasi), Cytomegolavirus na kadhalika.
Lakini pia mgonjwa akipungukiwa CD4
huweza kupata magonjwa ya mfumo wa fahamu yaani Central/Peripheral
Nervous System kama vile Cytomegolavirus, Toxoplasmosis, Cryptococcosis,
Mkanda wa Jeshi na Saratani.
Mengine ni magonjwa mbalimbali ya ngozi (Skin Diseases) hasa Saratani ya Ngozi.
Mengine ni magonjwa mbalimbali ya ngozi (Skin Diseases) hasa Saratani ya Ngozi.
Kutokana na uhaba wa vifaa vya kupimia kiwango cha seli aina ya CD4 katika nchi mbalimbali, Shirika la Afya Duniani (WHO), limetengeza mwongozo mwingine ambao utamsaidia mhudumu wa afya kutambua kama mgonjwa amefikia hatua ya ugonjwa wa Ukimwi na anastahili kuanza tiba au la.
Mgonjwa wa Ukimwi hupitia hatua
zifuatazo kabla daktari hajaamua kumuanzishia tiba, yaani dawa za
kupunguza makali ya virusi vya Ukimwi na kurefusha maisha (ARV’S).
Hatua ya kwanza kitaalam huitwa Clinical Stage I ambapo mgonjwa kwa kawaida anakuwa hana dalili zozote za ugonjwa (Asymptomatic).
Hatua ya kwanza kitaalam huitwa Clinical Stage I ambapo mgonjwa kwa kawaida anakuwa hana dalili zozote za ugonjwa (Asymptomatic).
Lakini mgonjwa anaweza kuwa na uvimbe
katika tezi ambao hauondoki, kitaalam huitwa Persistant lymphadenopathy.
Hatua ya pili au kitaalam Cilinical Stage II ni pale mgonjwa
anapopungua uzito chini ya asilimia 10 ya uzito wa mwili bila sababu
maalum.
Lakini mgonjwa aliye na maambukizi
akifikia hatua hii hujikuta akiwa na magonjwa ya mara kwa mara kwenye
mfumo wa upumuaji kama vile kuumwa masikio, kinywa, tezi la koo yaani
Tonsillitis, Otitis media na Pharyngitis, wengine huita magonjwa
nyemelezi.
Mgonjwa pia anaweza kukumbwa na mkanda
wa jeshi (Herpes zoster) au kuwa na vidonda pembezoni mwa mdomo au
kwenye kinywa (Recurrent oral ulceration).
Anaweza pia kutokwa na vipele mwilini yaani kuwa na ugonjwa wa ngozi ambao kitaalam huitwa Seborrhoeic Dermatitis pia kuwa na maambukizi ya fangasi katika kucha.
Anaweza pia kutokwa na vipele mwilini yaani kuwa na ugonjwa wa ngozi ambao kitaalam huitwa Seborrhoeic Dermatitis pia kuwa na maambukizi ya fangasi katika kucha.
Hatua ya tatu huitwa Clinical Stage III
ambapo mgonjwa sasa hupungua uzito kupita kiasi kwa kuwa atakuwa
anaharisha zaidi ya mwezi mmoja na atakuwa na homa inayojirudiarudia kwa
zaidi ya mwezi mmoja.
Lakini mgonjwa huyo akifikia hatua hii
atakuwa na maambukizi ya fangasi kwenye kinywa na anaweza kujikuta
akiugua kifua kikuu kwenye mapafu, au kupata maambukizi hatari ya
vimelea vya bakteria hivyo kujikuta akiugua homa ya mapafu au ugonjwa wa
uti wa mgongo.
Hatua hii ni mbaya kwa muathirika wa
Ukimwi kwani anapata maambukizi katika mifupa na viungo vya mifupa yaani
jointi, pia huwa na upungufu wa damu mwilini.
Hatua ya nne ya mgonjwa wa Ukimwi huitwa Clinical Stage IV ambapo mgonjwa hudhoofika mwili na kupata homa kali sana ya mapafu (Pneumocystis pneumonia) inayojirudia na hujikuta akipata saratani ya shingo ya kizazi.
Mgonjwa hupata maradhi kwenye mfumo wa
figo au moyo yanayochangiwa na VVU na hukumbwa na maambukizi ya fangasi
katika mishipa ya kupitisha chakula mpaka kwenye mapafu na mishipa yake
ya kupitisha/kusambaza hewa mwilini.
Mgonjwa anaweza kupata ugonjwa wa kifua
kikuu (TB) na fangasi, mgonjwa pia hupata saratani ya kwenye tishu za
mwili na maambukizi kwenye mishipa ya fahamu yanayosababishwa na vimelea
aina ya Toxoplasma gondii. Mbaya zaidi hujikuta akipata maambukizi ya
VVU kwenye ubongo.
Mgonjwa akifikia hatua hiyo akapimwa na kuonekana ana
upungufu wa CD4 daktari atamuanzishia dawa za ARV’S.
0 comments:
Chapisha Maoni