Kuna msemo maarufu sana usemao "NI HERI UKOSEE KUJENGA NYUMBA LAKINI USIKOSEE KUOA AU KUOLEWA"
Karibu katika mada hii, imenibidi nikuletee mada hii kwa sababu kumekuwa na maswali mengi sana, vijana wanaotaka au waliokaribia kuoa au kuolewa kutaka kujua mke au mume wa kuoa wanatakiwa waangalie nini.
Ndoa ni taasisi nyeti sana, Taasisi hii ikiyumba basi jamii pia itayumba. tunashuhudia mambo mengi sana ambayo yanatokea kwenye jamii ambayo ni matokeo ya kuyumba kwa taasisi hii:
watoto wanaoishi kwenye mazingira hatarishi, mmomonyoko wa maadili, umasikini, nk. Haya ni baadhi tu ya matokeo ya kuyumba kwa taasisi nyeti ya ndoa.
maranyingi kuyumba, na kuvunjika kwa ndoa hua kunahusiana sana
na mwanzo wa mahusiano ya kuelekea kwenye ndoa, yaani namna ya kuchagua yupi wa kuoa au kuolewa naye.
Kabla hatujaaza kuangalia mada hii naomba nikupe kisa
kimoja kilichotokea kwangu kipindi bado nikiwa mtoto.
Kipindi hicho nilikuwa nikiugua mama alikuwa ananipa dawa ya miti shamba, alikuwa anaenda porini anachimba mizizi ya miti au majani halafu anakuja anaiponda ponda anailoweka kwenye maji au anaikausha anaisaga saga inakuwa unga. Kisha baada ya hapo alikuwa ananipa ninywe. Chakushangaza dawa hizo mara nyingi zilikuwa chungu sana halafu nikimwambia mama mbona dawa chungu hivi? Mama alikuwa anasema “Fumba macho tu mwanangu kunywa ili upone”. Nilikuwa nikifanya hivyo mara nyingi.
Kipindi hicho nilikuwa nikiugua mama alikuwa ananipa dawa ya miti shamba, alikuwa anaenda porini anachimba mizizi ya miti au majani halafu anakuja anaiponda ponda anailoweka kwenye maji au anaikausha anaisaga saga inakuwa unga. Kisha baada ya hapo alikuwa ananipa ninywe. Chakushangaza dawa hizo mara nyingi zilikuwa chungu sana halafu nikimwambia mama mbona dawa chungu hivi? Mama alikuwa anasema “Fumba macho tu mwanangu kunywa ili upone”. Nilikuwa nikifanya hivyo mara nyingi.
Kisa hicho ni mfano halisi wa vijana wengi wanapoingia kwenye swala la kuoa au kuolewa. Nimewasikia vijana wengi wakisema heri nioe mwanamke wa aina hii kwa sababu nikioa wa aina hii watakuwa wananiibia watu wengine. Utakuta kijana kaoa au kaolewa na mtu ambaye mara nyingi kwenye mambo yao “anafumba macho tu ili apone”. Mimi nauliza kwanini uishi maisha hayo? Wakati kunauwezekano wa kupata mke au mume mzuri unayempenda?
Je, Wazee
wa zamani walikuwa wanaangalia sura au tabia?
Tunatakiwa kujifunza kutoka kwa wazee wetu, maana
wahenga wanasema ya kale dhahabu.
Tukianza kwa mfano Ibrahimu alimwoa Sara, Sara alikuwa
mwanamke mzuri sana wa sura na umbo na mcha Mungu, ndio maana Farao alimtamani
ingawaje Sara alikuwa mzee wa zaidi ya miaka 75.
Vivyo hivyo Isaka alimwoa Rebeka maandiko yanasema
alikuwa mzuri wa sura na umbo na mcha Mungu.
Yakobo alimwoa Raheli maandiko yanasema alikuwa mzuri
wa sura na umbo na mcha Mungu.
Mfalme wa Wakaldayo Ahasuero alimwaoa Esta maandiko
yanasema alikuwa mzuri wa sura na umbo na mcha Mungu.
Yoakimu alimwoa Suzana maandiko yanasema alikuwa mzuri
wa sura na umbo na mcha Mungu.
Wazee wa makabila mengi hapa nchini walikuwa wanawashauri
vijana wao wa kiume kuoa msichana mwenye sura nzuri na tabia nzuri.
Msichana
au mvulana mwenye sura nzuri ni yupi?
Binadamu wote tumeumbwa kwa umbo linalofanana, ingawaje
mwonekano wa mtu mmoja na mwingine hutofautiana. Tofauti hii ya mwokenano ndiyo
imebatizwa kwa majina ya sura nzuri na sura mbaya lakini wote ni binadamu wale
wale. Kwahiyo kwenye swala la kuoa au kuolewa mtu huchagua mtu wa kumwoa au
kuolewa naye mwenye sifa anazozitaka yeye na kwa sababu alizonazo yeye. Kwenye
swala la kuangalia sura nzuri au mbaya hiyo ni mitazamo tu (perception) ya
binafsi.
Nasema ni mitazamo ya binafsi kwa sababu mtu unayemwona wewe ni mzuri wa sura, mtu huyo huyo anaonekana kwa mwingine sio mzuri kama unavyomwona wewe. Ingawaje kuna mtu anaweza kuwa ni “popular” yaani anakubalika na wengi kwamba anasura nzuri lakini sio watu wote watakao kubali kuwa anasura nzuri.
Nasema ni mitazamo ya binafsi kwa sababu mtu unayemwona wewe ni mzuri wa sura, mtu huyo huyo anaonekana kwa mwingine sio mzuri kama unavyomwona wewe. Ingawaje kuna mtu anaweza kuwa ni “popular” yaani anakubalika na wengi kwamba anasura nzuri lakini sio watu wote watakao kubali kuwa anasura nzuri.
Kwa kifupi sura nzuri au sura mbaya ni mtazamo wa
binafsi, yaani ni hivi watu wote wanaweza wakasema huyu anasura mbaya lakini
ukimwamgalia wewe unamwona anag’aa kama malaika utabaki unawashangaa tu
wanaosema anasura mbaya.
Unapotaka
kuangalia tabia ya mtu angalia mambo yafuatayo
Naomba tuangalie baadhi ya mambo yanayoonesha tabia ya
mtu.
Jinsi
anavyo vaa.
Mavazi ya mtu na namna anavyoyavaa unapata kumfahamu
moja kwa moja jinsi alivyo mtu huyo. Sina haja ya kueleza sana namna uvaaji na
aina za mavazi jinsi yanavohusiana na
tabia ya mtu husika, ukweli ni kwamba mavazi na uvaaji wa mtu unaonesha tabia
ya mtu huyo. Kwako wewe unayeoa au kuolewa chunguza mavazi anayovaa mtu unayetaka
kuwa na mahusiano naye halafu utaamua sasa uoe au uolewe naye.
Jinsi anavyoongea
Maneno ya mtu huakisi kile kilichomo moyoni mwake.
Huhitaji kuhangaika wewe msikilize tu anapenda kuongelea mambo gani, basi,
utapata kumfahamu moja kwa moja. Mfano unaweza kumwuliza unapenda miziki gani
atakwambia halafu chunguza kama hiyo miziki na wewe unaipenda kama huipendi
maana yake hayuko upande wako. Jinsi mtu anavyoongea sauti yake na maneno
yanayotoka moyoni mwake ndivyo alivyo mtu huyo. Sikiliza sana maneno anayoongea
utaupata ukweli wote wa mtu huyo.
Jinsi
anavyoonekana.
Tabia ya mtu imefichwa kwenye sura ya mtu. Mfano mara
nyingi watu utawakuta wanasema huyu ni jambazi ukiwauliza kwanini watakwambia
huoni hata sura yake?. Mwonekano wa sura ya mtu mara nyingi ndivyo alivyo mtu
huyo. Chunguza sana sura ya mtu unayetaka kuwa nae kwenye mahusiano yako
utapata kufahamu vyema jinsi alivyo mtu huyo.
Jinsi
anavyotembea.
Kutembea kwa mtu kunamwonesha jinsi mtu huyo alivyo.
Kama mtu anatembea kwa madaha mengi, mwendo wa kubinuka binuka, mikono yake
haitulii mara huku mara huko kusiko kawaida unapata kujua kichwani mwa mtu huyo
kuna nini. Tembea ya mtu inawonyesha jinsi alivyo.
Jinsi
anavyotabasamu na kucheka.
Tabasamu la mtu na kucheka kwake kunamwonyesha jinsi
alivyo. Mfano kuna mtu mwingine ili atabasamu au acheke ni mpaka umempa noti,
au utakuta mtu anatabasamu lakini unagundua kabisa anafanya unafiki. Chunguza
tabasamu na kicheko cha mtu unayetaka kuingia naye kwenye mahusiano.
Sasa
uoe au uolewe kwa kuangalia sura au tabia?
Mimi nakushauri uoe au uolewe na yule mnayependana.
Sura na umbo zuri sio cha lazima ingawaje ni kitu muhimu kukiangalia na
kukizingatia. Nasema hivyo kwa sababu usifanye kama mama alivyokuwa ananiambia
“Fumba tu macho kunywa”.
Kama wewe ni mwanaume na huwa unapendelea wasichana wa aina fulani hivi, basi tafuta msichana wa aina hiyo hiyo halafu uoe. Usikubali kumwoa yule usiyempenda maana siku za baadaye utatamani kutafuta mwingine.
Mfalme Ahasuero alikuwa na uwezo wa kuoa msichana yeyote aliyekuwa anataka lakini aliwakusanya wasichana wote wazuri halafu akamchagua Esta msichana bikira, mzuri wa sura na umbo zuri. Huyo ndiye aliyempenda.
Inawezekana ningekuwa mimi au ungekuwa wewe usingempenda Esta. Ndivyo ilivyo kwenye swala la kuoa au kuolewa, chagua unayempenda.
Kama wewe ni mwanaume na huwa unapendelea wasichana wa aina fulani hivi, basi tafuta msichana wa aina hiyo hiyo halafu uoe. Usikubali kumwoa yule usiyempenda maana siku za baadaye utatamani kutafuta mwingine.
Mfalme Ahasuero alikuwa na uwezo wa kuoa msichana yeyote aliyekuwa anataka lakini aliwakusanya wasichana wote wazuri halafu akamchagua Esta msichana bikira, mzuri wa sura na umbo zuri. Huyo ndiye aliyempenda.
Inawezekana ningekuwa mimi au ungekuwa wewe usingempenda Esta. Ndivyo ilivyo kwenye swala la kuoa au kuolewa, chagua unayempenda.
Tabia ni kitu kingine cha muhimu sana kwa sababu unaweza ukangalia sura ukasahau tabia, utajuta. Ndiyo maana vijana wengi huwa wanasema sitaki kuolewa au kuoa na mvulana au msichana mzuri maana nitakuwa nagawana na wengine. Mimi hiyo naiita imani potofu. Wapo wasichana wazuri na wavulana wazuri wenye tabia nzuri labda sema ni uvivu wako tu wa kutafuta.
Kumbuka, ni afadhali umwoe mtu unayempenda na anayekupenda. Kama mmoja atapenda na mwingine hapendi, hiyo nayo ni shida itawasumbua sana.
0 comments:
Chapisha Maoni