Makosa ya wengine ni kitu cha kipekee sana kwetu, Makosa ya wengine yanaonekana haraka sana, kuliko hata makosa yetu. Makosa ya wengine yanatupa vitu vya kujadili na kukosoa.
Makosa ya wengine yanatupa ahueni kwamba angalau sisi tuko vizuri, kuliko hao wenye makosa hayo.
Makosa ya wengine tunaweza kuamua kuyatumia tutakavyo, kwa faida zetu binafsi.
Tunapenda kuongelea makosa ya wengine kuliko ya kwetu, lakini hili halifanyi makosa yetu kuwa madogo kuliko ya wengine. Na wala halipunguzi
makosa yetu sisi.
Makosa ya wengine tunaweza kuamua kuyatumia tutakavyo, kwa faida zetu binafsi.
Tunapenda kuongelea makosa ya wengine kuliko ya kwetu, lakini hili halifanyi makosa yetu kuwa madogo kuliko ya wengine. Na wala halipunguzi
makosa yetu sisi.
Acha sasa kutumia sana makosa ya wengine kwa faida zako binafsi. Weka nguvu zako kwenye makosa yako. Angalia ni yapi umeshindwa kufanya au umefanya kwa makosa. Na kisha fanya marekebisho.
Kama kuna makosa unaona wengine wamefanya, unaweza kujifunza kupitia makosa hayo, lakini siyo
kuyatumia kwa njia nyingine yoyote. Na kama unaweza kuwa msaada kwa wale waliofanya makosa, fanya hivyo.
Njia nyingine yoyote utakayoitumia kwa makosa ya wengine ni njia batili, haitakusaidia wewe wala yule
aliyefanya makosa. Badala yake itakuwa na madhara hasi, kwako unayeongelea makosa hayo utasahau yako, na kwa yule unayemwongelea makosa yake ataogopa hata kujaribu kufanya mambo makubwa, au kukata tamaa.
CHUKUA HII:
UKWELI NI KWAMBA ni rahisi sana kufuatilia na kujadili makosa ya wengine kuliko makosa yako binafsi. Lakini kujadili makosa hayo hakuna msaada wowote kwako au kwa mwenye makosa. Jaribu kuanzia sasa kuacha kutumia makosa ya wengine kwa faida zako binafsi. Badala yake jifunze kupitia makosa haya na kuwasaidia pale unapoweza.
“Freedom is not worth having if it does not include the freedom to make mistakes.” ― Mahatma Gandhi
(Hakuna maana ya kuwa na uhuru kama uhuru huo haukupi nafasi ya kufanya makosa.)
Kufanya makosa ni sehemu ya maisha yetu ya kila siku. Usikazane kuangalia tu makosa ya wengine, angalia makosa yako na yafanyie kazi.
0 comments:
Chapisha Maoni