Ndugu na rafiki yangu, sina hakika na hali yako kiuchumi kwa sasa iko je, unaweza kuwa na hali nzuri kiuchumi au hali inaweza kuwa sio ya kuridhisha au unaweza kuwa na hali mbaya kabisa.
Watu wengi hapa Tanzania wamekuwa wakilalamika kuwa maisha ni magumu.
Sikubaliani moja kwa moja na maneno hayo labda kwa shingo upande hivi naweza
kukubaliana na maneno hayo. Ninachokijua mimi ni kwamba maisha ni mazuri sana tena
ni marahisi sana. Mtu akisema maisha ni
magumu, ugumu wake unasababishwa na
kutokujua cha kufanya ambacho kinaweza kukuletea pesa.
Ziko mbinu lukuki za
kukuletea pesa, zina hitaji mtaji kidogo tu wakati mwingine bila hata mtaji. Kinachotakiwa
ni kupata ufahamu kidogo tu wa namna ya kufanya na ukitekeleza, tayari unaanza
kubadilisha maisha yako. Unaanza kuvuna pesa.
Kuna dunia mbili japo watu
wote tunaishi kwenye dunia hii hii moja. Wewe unapolalamika pesa hakuna, mtu
mwingine ,tena anaweza kuwa jirani yako anashangaa kuona jinsi pesa zilivyo
nyingi. Kwahiyo, wewe unaiona dunia haina pesa, jirani yako anaona dunia imejaa
mapesa mengi.
Kutafuta
Pesa Ni Mchezo
Usitafute pesa kama
unatafuta maisha. Tunajua mtu anapokuwa anaumwa huwa tuko makini kuhakikisha
anapona haraka, lengo la kupona ni
ili awe na maisha yake maana asipopona anapoteza maisha yake.
ili awe na maisha yake maana asipopona anapoteza maisha yake.
Unapotafuta pesa,
usitafute kama unatafuta maisha.
Tafuta kama unacheza mchezo.
Kama umeshawahi
kucheza mchezo wowote katika maisha yako utakuwa unafahamu hiki ninachosema. Lengo
la mchezo wowote ni kufurahisha, kuburudisha, kujenga afya na kushinda.
Unapokuwa
unacheza uwanjani unajisikia raha, unajisikia amani na hata ukitoka uwanjani
bado unajisikia vizuri kwa sababu mchezo unafurahisha, unaburudisha na unajenga
afya, lakini pia unaleta ushindi.
Kuna aina nyingi sana za
michezo duniani. Kuna mchezo wa mpira wa miguu, kuna mpira wa pete, kuna golf,
kuna mpira wa wavu, kuna mchezo wa magari, kuna mchezo wa ngumi nakadhalika. Pia,
kuna mchezo wa kutafuta pesa.
Kutafuta pesa ni mchezo
sawa na michezo mingine, huwezi kushinda mchezo wowote bila kufanya mazoezi,
huwezi kupata pesa bila kufanya moja wapo
ya njia za kupata pesa. Katika maisha yako usiangalie tu kazi moja ya
kufanya yenye kukuletea pesa unatakiwa kungalia kila kona kama vile mchezaji wa
mpira wa miguu, uwanja wote ni wa kwake.
Kama vile unavyocheza kwa furaha,
tafuta pesa kwa furaha hata pale unapokosa usihuzunike, jifunze, kisha songa
mbele. Ukitafuta pesa kwa jaziba huipati
ng’o au unapata kiduchu halafu unaweza kupunguza hata siku zako za kuishi kwa
sababu ya mawazo.
Lakini ukitafuta pesa kama mchezaji, kwanza utaufurahia mchezo, utaburudika moyoni mwako, utafarijika na bado utakuwa na afya njema na kadri unavyocheza ipo siku utakuwa mshindi, hapo ndipo raha ya kucheza itakapo kamilika.
0 comments:
Chapisha Maoni