Kuongozwa na hisia badala ya akili ni lazima utakuwa ni
mtu usiye na msimamo katika maisha yako. Leo utapanga hiki na kesho utapanga
kile lakini hutatimiza hata moja au hata kama utatimiza ni kwa kuchelewa sana.
Mambo
mengi ya maana utayapuuzia kwa sababu akili haitakuwa na nguvu ya kutenda
unachokitaka na badala yake hisia za wakati ule ndizo zitakazoamua nini
ukifanye. Chukulia kwa mfano: Unaongozwa na hisia ya ulevi, kila utakapoona
pombe lazima utakunywa tu kwa sababu akili haina nguvu yakupinga. Ukilewa, na
hisia ya ulevi ikiisha unaanza kujuta kwa nini umekunywa pombe.
Vivyo hivyo na
mambo mengine utajikuta unapelekeshwa na hisia zako badala ya akili zao, hapo
kufanikiwa kwako ni shida sana.
Nini
Ukifanye Ili Kutibu Ugonjwa Huu?
Kuifanya akili yako iwe na nguvu kuliko hisia zako sio
jambo rahisi. Ni kazi ngumu sana. Inahitaji muda na ubunifu mkubwa ili kutibu
ugonjwa huu. Jiulize ni mara ngapi umejikatalia au umejinyima kufanya mambo fulani
lakini bila kujua umejikuta unarudia kufanya mambo yale yale usiyoyapenda? Umetumia
mbinu ngani kuishinda hali hiyo lakini mpaka sasa
bado hujafanikiwa? Unafikiri dawa yake ni nini?
bado hujafanikiwa? Unafikiri dawa yake ni nini?
Mimi ninapendekeza Tiba Aina Mbili Kutibu Ugojnwa Huu.
Tiba
ya kwanza; Fanya kikao kila siku na watu waliofanikiwa
ili waiimarishe akili yako na kuzifisha hisia zako. Hii ni mbinu ngeni kabisa kwa watu wengi lakini ni mbinu kabambe
kabisa ya kutibu ugonjwa wa kuongozwa na hisia badala ya akili.
Unachotakiwa kufanya
ni kuchagua watu wawili au watatu haijalishi umbali waliko hapa duniani, wewe
ikifika kwa mfano jioni kabla ya kulala waarike watu hao kwenye kikao cha dakika
kumi. Unatakiwa kuwaalika kwa njia ya taswira unawaita kwa maneno unawahoji kwa
maneno tena kwa sauti kumbuka katika ulimwengu wa roho hakuna umbali. Unapofanya
hivyo taratibu utaanza kuishi kama wao walivyoishi/wanavyoishi.
Unapowaita kwenye
kikao wataje mmoja mmoja kwa jina lake na umuulize yeye amewezaje kufika hapo
alipofika? Tafakari juu ya maisha yao na ili uweze kutafakari juu ya maisha yao
unatakiwa ufahamu kwa undani juu ya maisha yao. Mbinu hii ni mzuri sana kuua
hisia zenye kukuharibu na huifanya akili yako ikuongoze badala ya kuongozwa na
hisia.
Hii itakusaidia kuongezeka kwa
kiwango kikubwa kuitumia akili yako kukuongoza badala ya kuongozwa na hisia
zinazopeleka upotevuni.
Tiba
Ya Pili: Jenga akili yako kwa kuangalia video au kusoma vitabu au kwa kusikiliza
rekodi za watu waliofanikiwa kila siku. Hakikisha unajiepusha kangalia mambo
yanayochochea hisia zako kuwa na nguvu kuzidi akili yako.
Hisia ikiwa na nguvu
hata kama ni kwa mambo mazuri bado utakwama baadhi ya mambo muhimu ya kutumia
akili. Kwahiyo kama una video ya mtu aliyefanikiwa iangalie mara kwa mara ili
akili ipate nguvu na kuzipiku hisia.
Mbinu hii unatakiwa uifanye kila siku ili
kupata matokeo mazuri haraka, kushindwa kufanya hivyo utasahau na matokeo yake
hisia zitakuongoza.
Usipoutibu
Ugonjwa Huo Mapema Nini Kitafuata?
Jambo kubwa litakalokupata ni kuchelewa au kushindwa
kabisa kufikia mafanikio yako. Utajifunza mengi hutafanyia kazi hata moja kwa
sababu hisia zitakuwa zinakupangia jambo lingine la kufanya badala ya lile
ulilojifunza. Pia utajifunza mambo mengi lakini utadharau mafunzo na kuanza
kutafuta mengine huku wenzako wakiyafanyia kazi mafunzo yale yale na
kufanikiwa.
0 comments:
Chapisha Maoni