MAGONJWA YA ZINAA YANAYOSABABISHA KUZIBA KWA MRIJA WA MKOJO

 
Dalili, mtu mwenye tatizo hili anaweza kuwa na dalili zifuatazo, 

kwa mwanaume hutokwa na manii zilizochanganyika na damu, kukojoa mkojo mweusi au uliochanganyika na damu, kutoa mkojo kidogo sana tena kwa shida, kukojoa mara kwa mara na kushindwa kumaliza mkojo wote. 

Wengine huona dalili za mkojo kujitokea wenyewe, hivyo mhusika kujikojolea, kusikia maumivu wakati wa kukojoa au chini ya tumbo au kwenye kinena, mkojo kutawanyika ovyo wakati wa kukojoa na uume kuvimba. 

Daktari akiona moja ya dalili hizo mgonjwa anaweza kuchunguzwa kwa vipimo tofauti kama vile kile cha kuchunguza mrija pamoja na kibofu cha mkojo (cystoscopy), kuangalia kiasi cha mkojo kinachobaki katika kibofu baada ya mkojo kutoka, X-ray ya mrija wa mkojo (Retrograde urethrogram) atapimwa kama ana magonjwa ya zinaa.

0 comments: