KILIMO
CHA NYANYA
Ndio, kilimo cha nyanya. Tembea
kila kona ya Tanzania, nyanya inaliwa kila mahali, kwa hiyo kulima nyanya
utakuwa na uhakika wa kupata soko. Nyanya inastawi katika maeneo mengi nchini
hivyo ukilima katika eneo ulilopo unaweza kupata mavuno mengi. Kilimo cha
nyanya kinawatajirisha watu wengi, hilo nimejiridhisha nalo sina wasiwasi.
Nakushauri uanze kulima
nyanya mwezi huu wa Septemba ili kufikia mwezi wa kumi na mbili uanze kuvuna na
upate million tano yako.
Mimi nimeamua kulima
nyanya; maandalizi ya awali yamekamilika ikiwa ni pamoja na kuandaa shamba la
ekari moja, kusia mbegu za nyanya na kutafuta mbolea ya samadi, yote hayo
tayari nimeyafanya; sasa naenedela kuandaa
shamba wakati mbegu zinakua.
Tukutane
Mwezi Disemba Nikuonyeshe Milioni Tano Yangu
Sikutanii wala sijisifii,
nataka nikuone na wewe unachukua hatua uanze kucheza mchezo wa kutafuta pesa. Sipendi
kukuona ulalamika na kunyong’onyea kisa huna pesa, nataka nikuone unafanikiwa,
ndiyo furaha yangu ndiyo maana nakueleza mambo kama haya ambayo kwa kawaida ni
siri yangu. Lakini kwa vile nataka
nikuone unaanza kucheza mchezo huu hata kama ni kidogo itakuwa vizuri, ukirudia
tena utafanya makubwa zaidi.
Sitaki kusema maneno mengi,
ufuatao ni mchanganuo wa kilimo cha nyanya ninacholima mimi. Unaweza kuandaa wa
kwako utakapo anza kulima.
KILIMO CHA NYANYA
Awamu ya Kwanza:
Septemba 2015
S/No Mahitaji Idadi/Kiasi
Gharama Jumla
1.
Kulima shamba Ekari
1 40,000/=
2.
Kuandaa matuta Ekari
1
50,000/=
Jumla ya gharama zote za kuandaa shamba 90,000/=
3.
Kununua
mbegu Packet
4 28,000/=
4.
Kuandaa
kitalu cha kusia
mbegu na kumwagilia
mbegu
5m2 10,000/=
Jumla ya maandalizi ya mbegu 28,000/=
5.
Kupanda
miche shambani Ekari 1
50,000/=
6.
Mbolea
ya samadi Trip 5 25,000/=
7.
Kununua
jenereta 1 500,000/=
8.
Kumwagilia
(mafuta) Mara 10
250,000/=
9.
Kupalilia
Mara 2
20,000/=
Jumla ndogo 845,000/=
10.
Mbolea
ya kuzalishia (CAN) Kilo 10 50,000/=
11.
Madawa
ya kutibu magonjwa ya nyanya 40,000/=
12.
Kuvuna mara 4
100,000/=
Jumla
ndogo 190,000/=
JUMLA
YA GHARAMA ZOTE 1,163,000/=
Mavuno
ya nyanya kwa ekari moja ikitunzwa vizuri yanaweza kufikia tani arobaini (40) sawa
na madebe 2,200 ya lita ishirini. Lakini kutokana na mabadiliko ya hali ya
hewa, magonjwa na sababu nyingine, kiwango cha chini cha kuvuna nimeweka tani
kumi na nane (18) sawa na madebe 1000 ya lita ishirini.
Debe
moja la nyanya hapa Bariadi linauzwa kwa Tsh 10,000/=. Labda kutokana na mabadiliko ya bei sokoni,
bei ya chini ninayoweza kuuzia iwe Tsh 8,000/= kwa debe.
Nitavuna
jumla ya madebe 1,000 na kila debe nitauza kwa Tsh 8,000/=, nitapata jumla ya Tsh milioni nane 8,000,000/=.
Jumla
ya mauzo yote 8,000,000/=
Jumla
ya gharama zote 1,163,000/=
Jumla Ya Faida nitakayopata 6,837,000/=
JUMLA YA FAIDA NITAKAYOPATA KWENYE
MRADI HUU AWAMU YA KWANZA NI TSH 6,837,000/=
Huna Milioni Moja, Utafanyaje Kupata
Mtaji Wa Kuanzia?
Naomba
nikutoe hofu juu ya hilo, ukiangalia kwa makini kwenye jedwali la mchanganuo
hapo juu, utagundua kuwa gharama nyingi nilizozitaja ni za vibarua ukitoa
gharama za jenereta, kununua mbegu, mbolea ya kuzalishia na dawa za kutibu
magojwa. Gharama zingine unaweza kuziepuka kama utashiriki wewe mwenyewe kwenye
shughuli hiyo bila kutegemea vibarua.
Njia Nzuri Ya Kupata Shamba Na
Mahitaji Mengine
Mimi
wakati naamua kulima nyanya sikuwa na shamba la kulima, nilizunguka zunguka
huko kijijini nafuta shamba la kulima angalau ekari moja. Haikuwa kazi rahisi
wala sikufanikiwa kupata shamba kabisa. Baadaye nilimkuta mzee mmoja anashamba
zuri sana lenye rutuba na liko karibu na bwawa la maji. Nikaongea na mzee huyo
na kumwomba kama ataniruhusu niungane naye kulima nyanya, tuupanue mradi uwe
mkubwa zaidi. Nikampa maelezo mengine mengi nikamweleza faida atakazo pata,
hatimaye mzee akakubali. Kwa njia hiyo nikawa nimepata shamba bure na mbolea ya samadi ya bure maana mzee
anafuga ng’ombe. Gharama pekee ni kuisafirisha mbolea kuipeleka shambani. Kupitia
ushirika huo nilioupata japo sikuwa na mwenyeji hata mmoja, sasa ninauhakika
kila kitu kitaenda kama kilivyopangwa.
Njia Hii Aliitumia Rafiki Yangu Na
Akafanikiwa.
Kuna
rafiki yangu mmoja tumesoma naye kidato cha tano na sita pale Milambo High
School, kwa sasa yuko Mwanza amehitimu chuo cha SAUTI mwaka jana. Baada ya
kumaliza masomo, hakuwa ana fahamiana na mtu yeyote pale jijini Mwanza zaidi ya
marafiki zake tu aliosoma nao chuoni. Siku moja akaanza kutembea mjini
akitafuta fursa, akafika sehemu fulani hivi akamkuta mzee mmoja anafuga kuku
wachache wa kienyeji , rafiki yangu alipowaona hao kuku alifurahi sana. Akamtafuta
yule mzee akafanya nae mazungumzo ya kuupanua mradi akamwambia faida atakazo
zipata baada ya mwaka mmoja. Yule mzee alifurahi kweli akamkubalia rafiki yangu,
kazi ikaanza. Nakawambia mpaka sasa wanafuga kuku zaidi ya elfu nne ndani ya
miezi minnne tu, na wanatarajia kuwa na kuku elfu kumi na mbili ifikapo mwezi Disemba
mwaka huu.
Tumia Njia Hiyo Utafanikiwa Tu
Kama
mimi nimetumia njia hiyo na nimefanikiwa, kama rafiki yangu alitumia njia hiyo
na akafanikiwa na wewe tumia njia hiyo upate mahali pa kuanzia nina uhakika
utafanikiwa. Kumbuka kutafuta pesa ni mchezo, cheza kwa furaha, bila hofu moyoni mwako hakika utashinda na
kufanikiwa.
Mbegu Gani Ya Nyanya Nzuri?
Baada
ya kuuliza uliza watu wengi na wataalamu wa kilimo, wamenishauri nilime aina ya
Mwanga.
Wanasema ina mavuno mengi na ganda lake ni gumu na inavumilia
magojwa mengi. Mahali unapoishi ulizia nyanya aina gani inakubalika sokoni,
utapata jibu. Mbegu zingine nilizozikuta madukani ni Tanya, Cal J, Tengeru 97,
Iffa, Mkulima, Maoney maker na nyingine nyingi. Fanya utafiti wako ujue ni ipi
inafaa.
Tulime Pamoja
Nachukua
nafasi hii kukukaribisha uambatane nami kwenye kilimo hiki cha nyanya. Unaweza ukawa
na uzoefu mkubwa wa kilimo hiki tafadhali weka maoni yako hapa chini kwenye
kibox cha comment ili utusaidie na sisi ambao ndio tunaianza kazi hii au
unaweza kuniandikia kupitia email yangu morningtanzaniasite@gmail.com.
Pia wale watakao kuwa na maswali yoyote wanaweza kuniuliza kwa email hiyo au
kwa kuandika kwenye kibox cha comment.
“Kama
mimi nimetumia njia hiyo na nimefanikiwa, kama rafiki yangu alitumia njia hiyo
na akafanikiwa na wewe tumia njia hiyo upate mahali pa kuanzia nina uhakika
utafanikiwa”
0 comments:
Chapisha Maoni