Wakati natafakari maisha jinsi
yalivyo na wakati natafakari ufahari wa mwanadamu hapa duniani, ndipo
nilipopata kuelewa kwamba maisha ni kama maigizo ni kama uchekeshaji vile. Kwanini
nasema hivyo?
Nasema hivyo kwa sababu usipoangalia kwa makini unaweza kuishi
kwa kujisahau jinsi ulivyo badala yake ukaishi kwa taswira ya dunia ambayo
taswira ya dunia sio kitu halisi bali ni taswira tu au mtazamo tu. Ndiyo maana
nikapata kanuni rahisi ya maisha kwamba maisha yote hapa duniani is a
game yaani ni mchezo kama ilivyo
michezo tunayoifahamu hivi sasa.
Najua hujaelewa ninachosema,
ngoja nikupe mfano; kuna wakati nilipokuwa ndogo nilikuwa naishi kwa taabu sana
kwa sababu nilikuwa najiona mimi ni mfupi na mwembemba zaidi kuliko wenzangu, kila siku nilikuwa najilinganisha na wenzangu
na nilijiona mimi ni mdogo zaidi. Niliishi kwa unyonge sana kipindi hicho
sikuwana uhuru wa kusimama na kujidai mbele ya wenzangu.
Iko
mifano ya namna hiyo mingi;
nimekutana na watu wanajiita wazuri wa sura
au walembo, mara nyingi hujivunia sura yao nzuri na jinsi
wanavyofuatwafuatwa
na watu maarufu kwahiyo watu hao huringia uzuri wa sura zao nzuri.
Baadaye nikagundua
kuwa kumbe mtu anayeringia na kujivunia uzuri wa sura au urembo mpe
muda, ndiyo
mtu yeyote anayeringia uzuri wa sura yake au maumbile yake mpe muda,
anza kumpa miaka 5 kisha njoo umtazame uone uzuri wake ulivyo kisha
mwongezee miaka mingine 5 halafu njoo tena umtazame
uzuri wake, utagundua kuwa kumbe uzuri wa sura na umbo zuri ni taswira
ya dunia
hii taswira yenyewe si kweli bali ni uongo.
Tangu kipindi hicho
nilipogundua
falsafa hii sihangaiki tena na maumbile yangu wala sithubutu
kujilinganisha na
mtu yeyote, jinsi nilivyo najifurahia
sana.
Kilichonishangaza
Zaidi
Katika pita pita yangu nimekuja
kuona mambo ya kushangaza, mtu mzuri wa umbo na sura nzuri lakini eti ni kichaa
au ni mwizi au akili zake zimeshft kidogo au ana hali ngumu isiyoelezeka au sio
maarufu kama watu wengine. Jumla ya yote
hayo ni kwamba sura au umbile la mtu halina nafasi katika mafanikio yake hata
siku moja. Kwa maana nyingine kufanikiwa kwako hakutegemei mwonekano wako
kunategemea mambo haya matatu tunayoenda kuyaangalia hapa chini ambayo ni
LAZIMA uwe nayo ili uweze kufanikiwa kwa kiwango cha juu zaidi.
Jambo
La 1: Wekeza Kwenye Viungo Vyako
Mwl Nyerere tunamshukuru na
kumuenzi vizazi na vizazi si kwa sababu alikuwa handsome au kwa sababu alikuwa
baunsa ni kwa sababu aliwekeza kwenye KINYWA CHAKE. Tofauti ya Mwl Nyerere na
mimi iko katika maneno yetu. Alitumia muda mwingi kukifundisha kinywa chake
kijue namna ya kuongea na akafanikiwa,
sasa amekuwa akisema na sisi Watanzania kwenye kila hatua ya maamuzi ya
kitaifa. Wanasiasa wote wanawekeza katika vinywa vyao. Wanamuziki wanawekeza
katika vivywa vyao wahubiri na watumishi wa Mungu wanawekeza katika vivywa
vyao.
Bahati nzuri huhitaji mtaji mkubwa kuwekeza katika kinywa chako
kinachotakiwa ni wewe kuamua na iwe sehemu ya shauku (Passion) au Hobby yako. Kwa
kufanya hivyo tu mafanikio unayavutia
kwako. Kuwekeza katika kinywa kuna muunganiko wa viungo vingine baadhi ya
viungo hivyo ni kichwa na moyo.
Watu wengi zaidi maarufu na
waliofanikiwa duniani wamejifunza kuwekeza katika viungo vyao pekee. Wapo
waliowekeza katika miguu yao sasa ni wachezaji maarufu na wanamafanikio makubwa.
Je, wewe ndugu yangu unayesoma makala hii umewekeza katika kiungo gani cha
mwili wako? Ukiniuliza mimi hilo swali nitakujibu kwamba mimi nawekeza katika
kinywa na mikono yangu.
Ili niwekeze katika kinywa, mara nyingi sana nasimama mbele ya watu na kuzungumza
na watu, kila jukwaa ninalopata nafasi nalitumia kuongea ni matumaini yangu
kwamba baada ya muda si mrefu nitafanya mambo makubwa kwa ajili yangu na taifa langu
kwa ujumla. Natumia mikono yangu iniletee faida. Ngoja tuliagalie hili kwenye
jambo ya pili hapa chini.
Jambo
La 2: Jiweke Mwenyewe Kwenye Historia Kwa Faida Yako Na Vizazi Vijavyo.
Moja ya mambo yananyonishangaza
ni pale ninapoenda kwenye maduka ya vitabu au maktaba ya vitabu. Asilimia 80%
ya vitabu vimeandikwa na watu wa mataifa mengine. Vitabu vichache sana
vimeandikwa na watanzania. Natafakari sana je sisi Watanzania hatuna cha
kuandika? Kwanini wao tu ndio wawe wanaandika wakati mimi na wewe tupo tu. Nataka
nikwambie mikono yako unaweza kuitumia kukuingiza kwenye historia.
Vitabu tunavyofurahia
vya neno la Mungu vimeandikwa na watu kama mimi na wewe walipopata uvuvio wa
Mungu wakaandika vitabu hivyo, kwani wewe na mimi hatupati uvuvio wa Mungu?
Kwanini usitumie maisha yako hapa duniani kuacha nyayo za kuwafundisha wengine
jinsi ya kuishi? Kwanini watu wengi zaidi wasibarikiwe kwa kuwepo kwako hapa
duniani? Kwanini mikono yako usiitumie kama silaha ya kukuletea mafanikio yako kwa vizazi vyako?.
Unahitaji mtaji kiasi gani
ili uanze kuandika vitabu vya kuufundisha ulimwengu?. Ni dhahiri kwamba
hujaamua au huoni umuhimu wake. Ni nia yangu kukujengea ari na kiu uanze
kubadili fikira zako kisha ujiweke kwenye historia wewe mwenyewe.
Jambo
La 3: Ongeza Kipato Chako Kwa Kuanzia Kanuni Rahisi Hadi Ngumu.
Pesa inawafurukutisha watu
ulimwenguni kote. Mimi na wewe tunatamani tuwe na pesa nyingi iwezekanavyo. Kibaya
zaidi badala ya kutafuta pesa kwa kutumia mbegu iliyoweka ndani yetu ya
kutuletea pesa, watu wengi wamekuwa wanaruka ruka huku na huku ili tu wapate
pesa. Lakini kwa umri wangu nilioishi hapa duniani nimeanza kugundua kwamba
kupata pesa ni rahisi sana ukitumia hobby na passion yako.
Mtu anayekwepa
kutafuta pesa kwa kutumia hobby na passion yake maisha yake huwa magumu zaidi.
Kuna dada mmoja kutoka Uganda anaitwa KANSIIME yeye ni comedian amenivutia sana
kwa kazi yake hiyo ya kuigiza. Hakuanza na mtaji bali anachotumia ni kinywa
chake tu kutengeneza pesa. Maisha kwake ni rahisi anafurahia jinsi alivyo, pesa anaivuna kwa njia naweza kuisema nyepesi
ukilinganisha na njia nyingine. Hobby yake ameibadilisha kuwa pesa. Kwani wewe unashindwa kuibadilisha hobby yako iwe
pesa?
0 comments:
Chapisha Maoni