Rafiki Mpendwa, Bila
shaka umewahi kupita sehemu mbalimbali za mjini, mfano sokoni na maeneo
mengine. Katika kupita kwako kote huko, hujagundua kitu
wala hujawazia kitu au bidhaa yoyote.
Siku moja ukapata wazo la kununua
jiko la
mkaa. Ukaenda tena mjini kama kawaida yako, lakini leo hii unawazo la
kununua
jiko la mkaa. Ukafika sokoni ukashangaa kuona jinsi majiko ya mkaa
yalivyo
mengi lakini siku za nyuma ulikuwa unapita pale pale ila huyaoni au kama
uliyaona hukuyafikiria.
Unaamua kuangalia ili uchague jiko zuri
unalolipenda, unajisemea ngoja nizunguke zunguke sokoni nikiulizia bei
na pia
nikitafuta jiko zuri nitakalolipenda. Unaanza kuzunguka sokoni
unashangaa kuona
kumbe soko limejaa majiko ya mkaa mengi namna ile, kila sehemu ni majiko
ya mkaa
hatimaye unaamua kununua moja unarudi nyumbani.
Siku nyingine kama kawaida yako unapita mjini katika
tembea tembea yako, huoni kitu, kila jambo ni kawaida tu.
Siku moja
unaamua ununue usafiri angalau uanze na
pikipiki. Siku inafika unaenda mjini kama kawaida yako, lakini leo hii unawazo la
kununua pikipiki. Unashangaa siku ile unaona vituo vingi sana vya kuuzia piki
piki halafu unagundua kumbe mjini kuna pikipiki nyingi sana za kila aina.
Siku
hii unaanza kuona na kuelewa aina za pikipiki lakini siku zingine ulikuwa
hujali sana kuangalia aina za piki piki. Unajisemea, ngoja nizunguke zunguke
mjini nikitafuta pikipiki nzuri. Unaanza kuzunguka zunguka unashangaa kila
mahali mjini kuna kituo cha kuuzia pikipiki. Hatimaye unachagua ya kwako
unanunua unarudi nyumbani.
Nimekupa mifano hiyo miwili nikitaka kukueleza
kwamba umezungukwa na fursa nyingi sana kila mahali zimezagaa. Tatizo huna
macho ya kuziona fursa hizo, mpaka siku utakapo weka malengo ya kuona baadhi ya
fursa hizo utashangaa kuziona zimetapakaa kila mahali.
Weka
Malengo Yako Nikuonyeshe Jinsi Inavyokuwa
Unapoweka malengo maana yake unataka ufike sehemu fulani.
Ni kama mtu anaposafiri kwenda mbali labda mkoa au nchi nyingine atahitaji
ramani imwongoze ili afike huko salama. Malengo hayawekwi kichwani tu, malengo
yanaandikwa.
Ni lazima unapoweka malengo yaandike na ukisha yaandika yapitie
mara kwa mara ikiwezekana kila siku na hata unapotembea unatakiwa uwe nayo
kichwani na ufikiri namna ya kuyafanikisha.
Anga
Lote Limejaa Mawazo Ya Kukusaidia Malengo Yako
Hii ni siri ya ajabu sana. Michal Miszcuk katika kitabu
chake Be Happy then Live (unaweza
kubonyeza jina la kitabu hapo juu kukidownload bure) anailezea siri hii kwa
undani sana , anasema anga lote limejaa nguvu ya ajabu ambayo kazi yake ni
kuwasaidia watu katika hisia zao.
Kama wewe unahisia za woga, nguvu iliyopo
angani itakuongezea woga mwingine ili uwe mwoga zaidi. Kama unawaza jambo fulani
na unakiu ya kutaka kulipata, uwe na uhakika nguvu ya angani itakupa majibu
haraka sana, ndio maana nimekupa hiyo mifano miwili hapo juu.
Kwahiyo,
ukitaka
kufanikiwa jambo lolote hata kama huna nyenzo za kulifanikisha jambo
hilo, usiogope
unachotakiwa wewe ni kuliandika liwe kama malengo yako halafu tumia
muda mwingi kuwaza na kufikiri namna utakavyolipata.
Kadri unavyo
waza na kufikiri ndivyo nguvu iliyoko angani inazidi kukufumbua macho
yako,
utashangaa siku zote ulikuwa unapita sokoni huoni majiko ya mkaa lakini
ukishawaza tu kununua jiko la mkaa macho
yako yanaanza kufumbuliwa taratibu unashangaa kuona soko zima limejaa
majiko ya
mkaa.
Ndiyo maana kama
usipoweka malengo hakuna kitu utakachofanikiwa au hata kama utafanikiwa ni kwa
kiwango kidogo sana, sisi hapa tunataka ufanikiwe kwa kiwango kikubwa.
Kichwa Chako Ni Kama Rada Hutuma Na Kupokea
Mawimbi
Brian Tracy katika
kitabu chake “The Goal” anaelezea jambo hili, anasema ndani ya
ubongo wa
mwanadamu kuna sehemu ndogo inayofanya kazi ya kutuma na kudaka mawimbi
kutoka
angani. Sehemu hii ya ubongo hutuma na kudaka mawimbi yale tu akili ya
mtu huyu inayawaza
kwa hisia kali au kwa kiu kali.
Kama unawaza kuwa mchawi na umedhamiria
kabisa
kuwa mchawi utashangaa siku moja moja unaota unaloga au unapaa na ungo,
ni kwa
sababu sehemu hii ya akili inadaka mawazo ya uchawi yanayoelea angani.
Kama
unawaza na unakiu ya kutengeneza ndege uruke angani, si ajabu unaweza
kutengeneza ndege yako, kama walivyofanya wale vijana wawili wa Marekani
waliotengeneza ndege ya kwanza, wanaitwa Wright Brothers.
Je, Wewe Unataka Nguvu Hii Ikusaidie Nini?
Chochote unachotaka
ikusaidie itakusaidia. Lakini masharti ya nguvu hii ni lazima uweke malengo ya
kile unachotaka ukusaidie, malengo yako yaandike halafu tumia muda mwingi
ukiyafikiria na kutaka kufahamu namna ya kuyafanikisha. Utashangaa kufumba na
kufumbua inakuletea jibu au njia.
Kumbuka sio lazima ikuletee majibu moja kwa
moja inaweza kukuletea mtu atakaye kupa mwongozo au inaweza kukuonyesha kitabu
cha kusoma chenye majibu ya kile unachokitaka.
Si ajabu hata mimi, ninaweza kuwa nimesukumwa na nguvu hii ili nikusaidie wewe kwenye kitu
unachokitamani na umekuwa unakitafuta muda mrefu. Sio ajabu, inaweza ikawa
hivyo.
Kama Mawazo Yako Angani Yanaelea, Chagua Moja
Ulifanyie Kazi.
Bila shaka, ulishawahi
kufikiria kuanzisha biashara fulani hivi. Kabla hujaanzisha hiyo biashara
unagundua kumbe kuna mtu mwingine ameianzisha tena inawezekana ni katika eneo
hilo hilo ambalo na wewe ulikuwa unafikiria kuanzisha.
Kwanini inakuwa hivyo?
Ni kwa sababu mawazo yote yapo angani yanaelea unapolidaka wewe kwa mfumo
nilioueleza hapo juu, na mwingine analidaka kwa mfumo huo huo.
Unatakiwa kufanya nini
basi?.
Robert Kiyosaki anasema usihangaike kubuni au kugundua bidhaa mpya.
Dunia imejaa bidhaa mpya nyingi sana lakini watu waliojidhatiti kufanya
biashara ni wachache sana. Maana yake nini?. Maana yake, biashara hiyo hiyo
uliyokuwa unaiwazia unaweza kuifanya lakini ukabuni mbinu ambayo wenzako hawana
na ukauza sana.
Kwa mfano, kuna rafiki yangu mmoja alikuwa anaelezea ubunifu
alioufanya jamaa yake sehemu fulani hivi, anasema yule jamaa yake alifungua
duka la bidhaa za umeme kama, luninga, suboofer, na vitu vingine vingi. Ili
kuteka na kupata wateja wengi, yule jamaa alianzisha mtindo wa kukopesha, kama
mtu akitaka kununua na hana hela ya kutosha au anayo kidogo alikuwa anamkopesha
kwa makubaliano maalum na mwisho wa mwezi analipa deni. Kwa kufanya hivyo alipata
wateja wengi sana na sasa ni tajiri mkubwa.
Anayefanya Vizuri Kuliko Wengine Ndiye
Mshindi
Dhamiria kuwa mshindi,
dhamiria kuuchukia na kuukataa umasikini. Fursa tunazo nyingi, uwezo wa
kufanikiwa tunao, kilichobaki ni kuweka nia ya kufanikiwa. Weka nia, hakuna
sababu ya kuwa masikini na tukiwa masikini ni kwa sababu hatutaki kufanikiwa,
sio kwa sababu hatuna nyenzo. Nyenzo tunazo tuzitumie, nyenzo ya kwanza ni
kuamua, nyenzo ya pili ni kupata maarifa na kutunza afya yako.
Ukiyazingatia
hayo kusanya nguvu nyingi kutoka angani halafu songa mbele. Usiangalie mtu
yeyote jiangalie wewe na hatima ya maisha yako. Hapa sio swala la kumwangalia
mume wako anasemaje wala sio swala la kumwangalia mke wako anasemaje, ingawaje
ni vizuri kama mtavipigana vita hivi pamoja.
Mimi nimeshachukua hatua, sitarudi nyuma, nakuhamasisha na wewe ujiunge
kwenye safari hii ya mafanikio.
imeandikwa na
0 comments:
Chapisha Maoni