Jumamosi, 9 Aprili 2016

Kiwango Cha Uhuru Na Kiwango Cha Kufikiri Vitakavyokuwezesha kupata mafanikio makubwa


Mungu anaupendeleo? Kwanini kuna watu wanaitwa ma-genius na wengine wanakuwa sio ma-genius? Unafikiri tofauti ni nini?. Je, wewe ni genius kama jibu ni ndiyo nakupongeza kama jibu ni sio kwanini sio genius?
 
Wakati natafakari somo hili nilishangaa sana kupata ufahamu ambao kipindi cha nyuma sikuwa nao. Nilirejea historia ya watu mashuhuri duniani ambao wameweza kufanya mambo makubwa yaliyosaidia kuufikisha ulimwengu mahali hapa. Baadhi yao ni  akina Sir Isack Newton, akina Bill Gate, akina Einstern Albert na wengine wengi. Ambao kila mmoja wao amefanya kitu cha kipekee kilichoushangaza ulimwengu.

Kwa kifupi na kwa lugha rahisi,  neno Genius ni mtu ambaye anauwezo wa kutumia akili yake kwa kiwango ambacho akili hiyo hiyo inampa matokeo makubwa au anatengeneza matokeo makubwa. Kila mtu anaakili lakini namna ya kuzitumia akili hizo tunatofautiana. Kwenye makala hii nalenga kuangalia namna au njia sahihi ambayo mtu anaweza kufanya ili aweze kufikia kuwa genius au aweze kujitengeneza yeye mwenyewe kuwa genius.

Chukulia kwa mfano; mimi nimeajiriwa ninauhakika wa kupata mshahara wangu mwisho wa mwezi. Wewe hujaajiriwa lakini unamiliki kampuni ya kutengeneza sabuni. Mimi nafanya kazi kwa kufuata mwongozo nilioukuta ofisini nilipoajiriwa. 
 
Wewe unajiandalia mwongozo wako mwenyewe lakini pia ili upate wateja wengi wa sabuni ni lazima ufanye ubunifu wa kipekee ili bidhaa yako iuzike sokoni haraka. Kwahiyo,  wewe muda mwingi zaidi unatumia kufikiri jinsi gani utapanua biashara yako lakini pia jinsi gani utaboresha bidhaa zako ili ziuzike sokoni. 
 
Bila shaka kwa sababu wewe ndiyo kila kitu kwenye kampuni yako,  utaishughulisha sana akili yako ili ikupe matokeo makubwa, kadri unavyoendelea kupanua biashara yako na kadri unavyoendelea kuboresha bidhaa zako ndivyo kiwango cha Ugenius kinavyoongezeka kwako. 
 
Hii ni tofauti kabisa na mimi niliyeajiriwa kwa sababu mimi nafanya kazi kwa kutumia mwongozo ambao nimeukuta ofisini, akili yangu sitaitumia kwa kiwango kikubwa kwani nafahamu hata kama mambo yasipoenda vizuri mshahara wangu upo pale pale. Matokeo yake sasa;  ni vigumu sana mimi kuwa genius,  zaidi nitabaiki kuwa mtu wa kawaida tu.

Wasomi Wetu Wako Wapi?
Kutokana na mfano huo hapo juu utashangaa sana wale waliokuwa vichwa darasani au waliokuwa wanafanya vizuri kwenye masomo,  ugenius wao hupotea haraka mara wapatapo kazi ya kuajiriwa. Hapa Tanzania tuna wasomi wengi ambao walikuwa magenius darasani lakini sasa hivi wapo wapo tu utawakuta wameshaajiriwa sehemu mbalimbali hawaishi kwa akili zao tena wanaishi kwa kufuata miongozo na masharti ya waajiri wao ugenius wao haupo tena.
 
Mambo Mawili Ya Kufanya Ili Kujitengeneza Kuwa Genius
Mambo yote yanawezekana ukiamua, kama hujaamua kuwa genius makala hii haitakufaa kitu lakini kama unakiu ya kuitumia akili yako ipasavyo ili ikuletee au ikutengenezee matokeo makubwa, unao uwezo wa kufanya hivyo. Kuna mambo mawili unatakiwa kuyafanya ili uweze kuwa genius mambo hayo ni haya yafuatayo;

Kiwango cha uhuru. Kujitengeneza kuwa genius kwenye jambo lolote ni lazima uwe na uhuru wa kufanya hivyo. Ninaposema uhuru maana yake upate muda wa kujiamulia mambo yako mwenyewe bila kutegemea mtu mwingine. Unatakiwa kutafuta uhuru huo popote hapo ulipo. Unapokuwa na uhuru wa kufikiria na kufanya chochote upendacho hiyo ni hatua nzuri inayoweza kukutengeneza kuwa Genius.

Kiwango cha Kufikiri. Jambo la pili unalotakiwa kufanya ni kubadilisha mfumo wako wa kufikiri. Unatakiwa uwaze zaidi namna ya kuongeza ugenius. Unapoanza kuwaza namna ile utajikuta unapenda kujifunza zaidi kwa wengine waliotangulia hapo ndipo ugenius wako utajijenga na kukua. Unapokuwa na uhuru wa kufikiri kisha tena akili yako iko tayari kufikiria,  huo ni msingi imara wa kujitengeneza kuwa genius.

Kwa maoni yangu kila mtu anaweza kuwa genius akitaka. Kwanza awe na uhuru au muda wa kufikiria kuhusu kuwa genius pili awe tayari kuitumia akili yake ili iweze kumpa matokeo makubwa. Amua leo kuwa genius halafu utaona matokeo makubwa.


0 comments: