Neno Himaya linamaana zaidi ya moja lakini maana
ninayozungumzia hapa ni biashara kubwa(extensive) inayoongozwa na mtu mmoja au kampuni.
Mfano kwa Tanzania ni Himaya ya Said Salim Awadh Bakhresa.
Mpenzi msomaji wangu ninaamini kuwa makala
hii itakusaidia kukutia hamasa ikiwa unandoto za kufika mbali kiuchumi. Hakuna
kazi ngumu kama kujenga kitu kikubwa kisichokuwepo na ambacho wewe ndiye
mwanzilishi wake. Inahitaji juhudi kubwa, maarifa mengi, uzoefu wa kutosha,
ubunifu mwingi na zaidi ya hayo inahitaji maono dhahiri.
Dr.Laura Schlessinger, Mwandishi wa vitabu na mtoa
maada wa vipindi vya redio huko Marekani aliwahi kusema “Usijaribu kufanya jambo lolote
ikiwa haujajiandaa kukabiliana na changamoto zinazotokana na jambo hilo”.
Mimi nasema usijaribu kuanza kujenga himaya yako ikiwa hauna kiu ya dhati
ya kuwa na himaya. Ni gharama kubwa zinahitajika sio gharama za pesa tu bali na
gharama ya muda, mawazo,elimu,na ushindani nk.
Elimu yako ya darasani inaweza kukusaidia kidogo
sana kwenye ujenzi wa himaya hiyo. Nasema hivyo kwa sababu huku mtaani watu wengi waliofanikiwa kujenga himaya zao wengi wao hawajasoma sana. Kama wewe umesoma hiyo ni msaada wa ziada utakusaidia kwa namna moja au nyingine. Nitakupa mfano wa Said Awadh Bakhresa.
sana kwenye ujenzi wa himaya hiyo. Nasema hivyo kwa sababu huku mtaani watu wengi waliofanikiwa kujenga himaya zao wengi wao hawajasoma sana. Kama wewe umesoma hiyo ni msaada wa ziada utakusaidia kwa namna moja au nyingine. Nitakupa mfano wa Said Awadh Bakhresa.
Mapitio
ya Said Salim Awadh Bakhresa.
Bakhresa amezaliwa mwaka 1949 huko Zanzibar. Akiwa na miaka
kumi na nne (14) tu aliacha shule na akaanza kukaanga chips na baadaye
alifungua mgahawa wake maeneo ya kariakoo jijini Dar es Salaam.
Miaka ya 1970
aliweza kufungua mashine ya kusaga unga na mpaka sasa ana kiwanda kikubwa cha kusaga unga pale
Kipawa, Dar es Salaam. Kiwanda hicho kinaitwa “Kipawa Flour Mill” ambacho kinasambaza unga wa ngano na mahindi
Tanzania nzima na Afrika Mashariki kwa ujumla hasa katika nchi ya Rwanda na
Burundi
Said Salim Bakhresa ametumia miaka 30 ( miongo mitatu)
kujenga himaya yake ya biashara ambapo mpaka sasa kwa mujibu wa gazeti la Marekani
la Forbes la mwaka jana 2014 limemtaja Bakhresa akiwa na utajiri wa zaidi ya
dolla za kimarekani milioni 575, huku akiwa nafasi ya 44 kati ya matajiri 50 wa
kwanza barani Afrika. Katika makampuni yake yote anaajiri zaidi ya wafanyakazi
2000.
Kwa sasa ana miliki makampuni mengi huku kampuni la azam, likifanya vizuri zaidi sokoni.
Amejikita katika biashara ya kutengeneza vinywaji, chokoleti, na kutoa huduma ya vyombo vya
usafiri kama vile meli na magari,pia akiwa amewekeza kwenye sekta ya habari akiwa anamiliki kituo cha
luninga, na katika michezo hajabaki nyuma akiwa anamiliki timu ya mpira wa
miguu ya Azam FC. Hayo ni machache tu kwa kuyataja.
Kujenga
Himaya Yako Inawezekana.
Unaposema kujenga himaya, ni kitu kikubwa sana na ni
watu wachache wenye uthubutu wa kuchukua hatua kuelekea huko. Lakini utashangaa
watu wengi hata kule kuanzisha kile kidogo ni ngumu sana. Tatizo nini ni? Sio
rahisi kulijibu swali hili lakini ninachotaka ufahamu kuwa jambo lolote
linawezekana ikiwa kuna mambo haya mawili ya awali;
Wazo (Idea) na Kiu (Desire). Mambo hayo mawili ndiyo chimbuko la
mambo yote katika maisha ya mwanadamu. Ukikosa kimojawapo kati ya hivyo hakuna
kipya utakachokifanya, mfano ukikosa Wazo hata kama una Kiu kiasi gani
utashindwa ufanye kipi utatangatanga mara ujaribu hiki mara ujaribu hiki matokeo
yake ilikuwa asubuhi hatimaye inafika jioni yaani unazeeka bila kitu kipya
ulichofanya. Pia, ukiwa na wazo halafu ukakosa kiu ya kulitekeleza wazo hilo
kwa vitendo utakuwa ukienda kwenye makundi ya watu wanaozungumzia mawazo yao
unakuwa wa kwanza kuelezea “aisee yaani mimi
napanga kufanya hiki na hiki Mungu tu anisaidie” ukitoka hapo hutekelezi
hata kimoja.
Watu
Wengine Waliofanya Maajabu Katikati Ya Mazingira Yalioonekana Haiwezekani.
David Ben- Gulion Waziri Mkuu wa kwanza wa Israel
alitoa agizo kwamba kijengwe chuo kikuu katikati ya jangwa la Negev lililoko
kusini mwa Israel. Wananchi wa nchi ile walilalamika na kunug’unika wakisema
haiwezekani kujenga chuo kikuu jangwani hii haitawezekana kabisa, walisema
hivyo; lakini yeye aliendelea na msimamo wake wa kujenga chuo kikuu hicho.
Hivi
sasa hicho chuo kimeshajengwa na kinaitwa Be-Gulion University ni miongoni mwa
vyuo vikuu vichache duniani vinavyofundisha masomo na utafiti wa majangwa.
Alifanikiwa kwa kuwa na kiu na wazo ambalo aliamua kulitekeleza kwa vitendo ndio
maana alichukua hatua na alifanikiwa.
Kule Uholanzi, waliweza kutengeneza nchi mpya kwa kile
kinachoitwa Land Reclamation. Ni kitu cha ajabu kutengeneza nchi ndani ya
bahari lakini walifanikiwa.
Thomas Edson aliweza kutengeneza bulb za umeme ingawaje
alifeli mara elfu kumi (10,000) kabla ya kufanikiwa.
Kilichowasaidia hao wote
ni kiu na wazo kisha wakachukua hatua.
Mambo
Haya Yatakusaidia Na Kukutia Moyo Wakati Unapoanza Safari Yako Ya Kujenga
Himaya Yako.
Jambo la kwanza:
Tafuta Sababu Ya Kuwa Na Himaya Yako.
Sababu ya wewe kuwa na himaya ni muhimu sana unapotaka
kujenga himaya yako. Ndiyo itakuwa inakuchochea uwe na bidii ya kupiga hatua
zaidi kuelekea kwenye himaya yako.Baadhi ya sababu unazoweza kuzitumia kama
kigezo cha wewe kujenga himaya yako ni hizi zifuatazo; lakini unaweza kuweka za
kwako.
- Kusaidia watu wengi zaidi. Mfano kuna rafiki yangu mmoja alisema yeye anatamani sana katika himaya yake anayoijenga aje aajiri angalau watu miatatu (300) kwa sasa amefikisha watu miamoja (100).
- Kufanya chochote unachokitaka. Mfano kusafiri kwenda popote duniani, kumiliki aina yoyoye ya gari unaoitaka, kujenga na kuishi kwenye aina yoyote ya nyumba unayoitaka n.k
- Kwanini wawe wao na sio mimi?.hii ni sababu tosha ya kukufanya ujenge himaya yako. Kwanini wao tu waitwe matajiri halafu mimi niitwe masikini?. Nguvu ninazo, uwezo ninao fursa ninazo sasa kwanini wawe wao nasio mimi?
- Iwe ndo “hobby” yako. Ndiyo, ukiwa na himaya yako na ukaijenga vizuri inakuwa kama hobby fulani hivi. Kila unapotembea kutoka sehemu moja ya himaya yako kwenda sehemu nyingine unajisikia kuburudika zaidi au una “enjoy life”
- Njia mojawapo ya kumshukuru na kumtukuza Mungu. Unajenga himaya yako kwa lengo la kumpa sifa na utukufu Mungu wako. Ndivyo walivyofanya matajiri wa zamani kama Ibrahimu na Mfalme Sulemani.
Jambo la Pili: Weka
Kwenye Maandishi Na Kisha Andaa Ramani Yake.
Huwezi kujenga himaya bila mwongozo wa maadishi.
Unatakiwa uandike kila hatua utakayopitia. Kwa jina jingine inaitwa “Financial Plan”.
Kama hufahamu namna ya
kuandika financial plan tafuta mtu mwenye uelewa akusaidie kuandika. Financial
plan inakupa dira au mwelekeo wa namna ya kujenga himaya yako. Pia jambo kubwa
kabisa, inakuonyesha muda utakao tumia hadi kujenga himaya yenye nguvu. Kama
vile mtu anayejenga nyumba huandaa ramani, ramani hiyo sio tu kumwonesha fundi
vipimo bali pia inamhamasisha anayejenga kila aionapo anatamani zaidi aendelee
kujenga ili aikamilishe.
Bila ramani kunakukosea vipimo lakini pia hukatisha
tamaa maana huoni mwisho wake utakuwaje. Vivyo hivyo unapojenga himaya yako
lazima uandae andiko (financial plan) itakayo kusaidia kuiona himaya yako ukiwa
mwanzoni.
Jambo la Tatu: Chukua
Muda Kupata Maarifa Na Kutafuta Fursa.
Itahitaji muda kidogo kujifunza mambo muhimu ya awali
mfano sheria za uendeshaji biashara, namna ya uwekezaji, masoko na hesabu na
uhasibu. Mambo hayo ni muhimu unapotaka kujenga himaya yako. Pia kutafuta fursa
ni jambo ambalo unatakiwa ulipe kipaumbele ili utakapo anza kujenga himaya yako
uwe unajua fursa zipo sehemu gani, na itakuwa rahisi kwako kuzitumia.
Utajifunza
mambo hayo yote kwa kusoma vitabu, kufanya maongezi na watu wenye himaya
tayari, kuzungumza na watu wenye fani unazotaka kuzitumia mfano, wanasheria,
wahasibu, wafanyabiashara n.k. njia nyingine nzuri ni ya kutembelea miradi na
kujifunza namna ya uendeshaji wa miradi hiyo.
Jambo la nne: Kuna
kitu kinaweza kukutoa nje ya mstari
Kuna mambo mengi yanatakiwa kukamilishwa au mengine
utaendelea nayo huku ukiendelea kujenga himaya yako. Jambo la muhimu kabisa ni kulishika
ni nidhamu katika hatua hii. Tena, kumbuka kutunza afya yako ili ufikie malengo
yako. Tabia zozote zinazokutoa kwenye mstari wa ujenzi wa himaya unatakiwa
uziepuke au uziache.
Mungu ni muhimu sana kumshirikisha ili akutie nguvu za
kujenga himaya yako. Unatakiwa kujifunza
kila siku wakati wote ukiwa unajenga himaya yako kwa kusoma vitabu na kwa namna
yoyote itakayo kuongezea ufahamu na bidii ya kuendelea kujenga himaya yako.
0 comments:
Chapisha Maoni