Tabora New Hope Agency
Is aiming to improve the standard of living of the people in a community by planning on the utilization of the available resources and guiding on the implementation of the plans to achieve the best social services in Tanzania.
Tabora New Hope Agency
Is aiming to improve the standard of living of the people in a community by planning on the utilization of the available resources and guiding on the implementation of the plans to achieve the best social services in Tanzania.
Tabora New Hope Agency
Is aiming to improve the standard of living of the people in a community by planning on the utilization of the available resources and guiding on the implementation of the plans to achieve the best social services in Tanzania.
Tabora New Hope Agency
Is aiming to improve the standard of living of the people in a community by planning on the utilization of the available resources and guiding on the implementation of the plans to achieve the best social services Tanzania.
Tabora New Hope Agency
Is aiming to improve the standard of living of the people in a community by planning on the utilization of the available resources and guiding on the implementation of the plans to achieve the best social services Tanzania.
Alhamisi, 23 Agosti 2018
Kilimo Cha Nyanya
How They Think
Back How They Think Thousands of potential millionaires are born every year. And with the advent of e-commerce, making a million dollars is becoming more and more commonplace. What advice did the money-makers follow? Aristotle Onassis worked eighteen hours a day to maintain his fortune. He started as a welder and aimed for the top. "You have to think money day and night," he said, "you should even dream about it in your sleep." Do you? John D. Rockefeller, Jr., said, "I believe in the dignity of labor, whether with head or hand; that the world owes every person an opportunity to make a living." And J. Paul Getty acknowledged his hard work: "I have no complex about wealth. I have worked hard for my money, producing things people need." Even Proverbs advises: "In all labor there is profit." Richard Bach, the author of the best selling Jonathan Livingston Seagull wrote... "You are never given a wish without also being given the power to make it true. You may have to work for it, however." The Empress of the British Empire, Queen Victoria, admonished, "We are not interested in the possibilities of defeat." Back
JINSI YA KUFANYA MAHUSIANO YAKO KUWA BORA
Siku hizi kumekuwa na lawama nyingi kuhusiana na mahusiano ambapo kila upande umekuwa ukilaumu upande mwingine kuwa ndio chanzo cha kuvurugika kwa mahusiano yao, kibaya zaidi ni kwamba wakati mwingine upande unaokua unalalamika sana unaweza ukawa ndio upande uliochangia kwa kiasi kikubwa kuvurugika kwa uhusiano uliokuwepo
Japo kuna njia nyingi za kuboresha mahusiano kulingana na aina ya wahusika waliopo katika mahusiano, Zifuatazo ni baadhi ya njia ambazo unaweza kuzitumia kuboresha mahusiano yako.
Siku zote katika maisha unatakiwa ujitambue
Jumanne, 21 Agosti 2018
UZAZI WA MPANGO
Masuala ya uzazi na malezi kwa wanawake ni jambo lililo wazi kabisa lakini kutokana na maadili baadhi wamekuwa na woga wa kujadili wazi wazi. Hata vivyo baadhi ya wanawake hawa hupenda kuzungumzia maswala haya hasa wanapo kutana ili kubadilisha mawazo na hata kujifunza zaidi.
Watu 103 wakamatwa katika maandamano ya kupinga kukamatwa Bobi Wine Uganda
Vikosi vya usalama nchini Uganda vilizima maandamano kwenye mji mkuu hapo jana Kampala kupinga kukamatwa kwa Bobi Wine .
Waandamanaji wamechoma mot
DANGOTE KUMALIZA UHABA WA SARUJI
Kampuni hiyo imesaini mkataba wa kuuziwa gesi asilia kwa miaka 20. Kampuni hiyo inayomilikiwa na bilionea namba moja Afrika, Aliko Dangote wa Nigeria na Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC).
Kabla ya ahadi hiyo itakayoanza kutekelezwa katika
Waomba wasaidiwe umeme wa REA
Maombi hayo waliyatoa mwishoni mwa wiki katika mikutano ya hadhara iliyofanyika katika maeneo mbalimbali wakati wa ziara ya mbunge kukagua miradi hiyo na kuelezea namna Ilani ya CCM inavyotekelezwa. Wananchi wa mitaa ya Bolisa, Ukunku na Mulua, walimwomba mbunge wa Kondoa Mjini, Sannda kuwasaidia kupata huduma ya umeme katika mitaa yao ambayo imepitiwa na nguzo za umeme wa REA na haijapewa umeme.
Akijibu maombi hayo, mbunge huyo alisema, serikali imepanga kuhakikisha kwamba wananchi wote wanapata huduma ya umeme katika jimbo hilo. Sannda alisema, mkandarasi wa kusambaza umeme katika mitaa mbalimbali katika wilaya ya Kondoa tayari amepatikana, kinachosubiriwa sasa ni kuanza kazi baada ya kumaliza kazi katika wilaya ya Chamwino na Bahi. Sannda alisema serikali imeendelea kutenga fedha kwa ajili ya kutoa huduma hii na ndio maana inafanya kazi kwa awamu ambapo katika awamu ya kwanza kuna maeneo yalipata huduma ya umeme mengine hayakumalizika.
Alisema ilianza awamu ya pili ambayo ilikamilisha sehemu iliyobakia katika awamu ya kwanza na kuanzisha miradi mipya. Aidha aliwasihi wananchi hao kuendelea kutunza vigingi vilivyowekwa na Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) kama alama za kuweka nguzo kwani maeneo mengine wananchi wamekuwa wakiviharibu na kuwapa kazi wakandarasi wanapoanza kazi. Sannda aliwataka wananchi kuendelea kufanya maandalizi ya kusuka nyaya za umeme katika nyumba zao na kuajiandaa kuweka fedha za kulipia huduma ya kuingiza umeme katika nyumba zao.
Ziara ya Sannda ilifanyika katika kata zote nane za Halmashauri ya Mji Kondoa ambapo alifanya ukaguzi wa miradi mbalimbali na kufanya mikutano ya hadhara na wananchi wa maeneo hayo. Katika mikutano hiyo ya hadhara, wananchi walipata fursa ya kuuliza maswali ya utekelezaji wa Ilani ya CCM kwa kipindi cha miaka miwili. Katika ziara hiyo pia aliongozana na viongozi mbalimbali wa CCM katika Wilaya ya Kondoa na wataalamu mbalimbali kutoka katika Halmashauri ya Mji Kondoa.
Jumanne, 14 Agosti 2018
Mcheza filam wa Tanzania Monalisa atoa wito kwa wawekezaji kutupia jicho filam za Bongo.
Monalisa |
Jumatatu, 6 Agosti 2018
Mtanzania asherehekea miaka 100 ndani ya ndege ya Dreamliner
Isitoshe, amekuwa miongoni mwa Watanzania wa mwanzo mwanzo walioabiri ndege mpya iliyonunuliwa na serikali ya Tanzania kwa ajili ya kuliimarisha Shirika la Ndege la Taifa (ATCL) na kupokelewa mwezi uliopita.
''Mwanangu namshukuru sana kwa sababu aameweza kunipandisha kwenye ndege, nimefurahi sana..'' amesisitiza mzee Kimweri.
Akizungumzia zawadi aliyompa baba yake mtoto wa mzee Kimweri, Imam Dafa anasema ilimchukua muda kufikiria juu ya nini cha kumpa baba yake. ''Nilikuwa nafikiria kwa kumshukuru Mungu na kumpa baba zawadi kwa kufikia umri huo nifanye nini, nilifikiria sana, basi nikaona nimpe baba zawadi ya kupanda ndege kwa mara ya kwanza akiwa na umri wa miaka 100...'' alisema Imam.
Venezuela yailaumu Marekani jaribio la kuuwawa Maduro
Katika hotuba iliyopeperushwa moja kwa moja na vituo vya televisheni nchini Venezuela, Rais Maduro amesema kwamba kila ishara inaonyesha kwamba ni jirani wa Venezuela, Colombia, ndio mhusika mkuu wa jaribio hilo la kumuua na kuongezea kwamba Mungu, watu wa Venezuela na wanajeshi wake ndio waliomuokoa.
"Hiyo ndege yenye mabomu ilikuwa imenilenga mimi lakini kinga ya upendo iliniokoa. najua nitaishi miaka mingi zaidi," amesema Maduro.
Ndege yenye vilipuzi na isiyoruka na rubani, vililipuka majira ya saa kumi na moja dakika 41 Jumamosi jioni, wakati Maduro alipokuwa akihutubia umati wa maelfu ya wanajeshi katika uwanja wa mji mkuu wa Caracas.
Kwa mujibu wa shirika la habari la Ufaransa la AFP, Rais Maduro hakupata majeraha yoyote lakini wanajeshi saba walijeruhiwa.
Maduro amesema kwamba hana shaka kwamba Rais wa Colombia Juan Manuel Santos, anahusika na shambulizi hilo.
Shirika la habari la AFP linamnukuu afisa wa serikali ya Colombia akisema kwamba shutuma hizo dhidi ya Rais Santos "hazina msingi wowote"
Maduro amesema kuwa uchunguzi wa awali "unaonyesha kwamba wanaofadhili watu wanaotaka kumuuwa wanaishi katika jimbo la Florida nchini Marekani. "Ni matumaini yangu kwamba rais Donald Trump yupo tayari kupigana na hawa magaidi"
Kiongozi huyo wa Venezuela amesema kwamba watu kadhaa wanaopanga njama ya kumuua wamekamatwa, lakini hakutoa taarifa zaidi.
shambulizi lilitokea wakati Maduro alikuwa akizungumzia kuhusu uchumi wa Venezuela. video zinaonyesha Maduro na wengine wakiwa wameduwaa baada ya sauti ya milipuko mikubwa kadhaa kusikika. mda mfupi baadaye, video inaonyesha wanajeshi wakitafuta mahali pa kujikinga.
nchi ya Venezuela imekumbwa na mgogoro wa kisiasa kwa muda mrefu. Licha ya kuwa na utajiri mkubwa wa mafuta, uchumi wa nchi ya Venezuela umeporomoka, mfumuko wa bei ukikaribia kufika asilimia mia mojamwaka 2018, huku nchi hiyo ikikumbwa na mgogoro mkubwa wa kibinadamu pamoja na uhaba mkubwa wa bidhaa muhimu.
Katika siku za hivi karibuni, maelfu ya raia wa Venezuela wamelazimika kukimbilia nchi jirani kutokana na hali ngumu ya maisha nchini mwao.
Maduro alichaguliwa kuwa rais wa Venezuela mnamo mwezi Mei 2018 kutawala kwa mhula wa miaka sita katika uchaguzi ambao wanasiasa wa upinzani na waangalizi wa kimataifa walikataa matokeo yake, kwa msingi kwamba ulikumbwa na udanganyifu katika zoezi la kuhesabu kura.
Chini ya mkataba huo, Salva kiir atasalia kuwa rais, na Riek Machar kurudi nyumbani na kuwa makamu wa rais wa kwanza, huku nafasi tano za makamu wa rais zikiundwa.
Kutakuwepo serikali ya mpito ya miezi 8 itakayoongozwa na Salva Kiir, na baadaye serikali ya mpito ya miaka 3.
Kutokana na mkataba huo, serikali itakuwa na mawaziri 20 kutoka kwa chama cha Kiir, tisa kutoka chama cha Machar na sita kutoka makundi mengine.
Hii ndio hatua ya hivi karibuni kati ya hatua kadhaa zilizowahi kuchukuliwa kuleta amani nchini Sudan kusini tangu mwaka wa 2013.
Mkataba wa amani wa 2016
Mkataba wa amani ulivunjika July 2016 wakati mapigano yalipozuka katika mji wa Juba na kupelekea Machar kutoroka nchini kwa kupitia njia za vichakani.
Tangu mda huo, amekuwa chini ya kifungo cha nyumbani nchini Afrika kusini.
Serikali ya Sudan Kusini inasisitiza kwamba mara hii, mambo yatakuwa tofauti kati ya viongozi hao wawili na kwamba Machar amejifunza "kupitia hali ngumu" na kwamba ameahidi kushirikiana na Kiir kwa sababu hataki kurudi nchini Afrika kusini.
Katika kikao na waandishi wa habari, msemaji wa serikali ya Sudan kusini Michael Makuei amesema kwamba wapiganaji wa Salva Kiir watapewa mafunzo na kujiunga na jeshi la taifa.
Mkataba huo ni hatari?
Mchambuzi wa siasa za Sudan Kusini Alan Boswell ametaja mkataba huo kuwa hatari.
"Mnamo mwaka 2013, Riek alitaka kuchukua nafasi ya Kiir lakini Kiir alijibu kwa nguvu zote na kumfukuza serikalini. Mwaka 2016, hali ilikuwa hivyo hivyo. Matokeo hayo mawili yalisababisha vita vikubwa. Mkataba huu wa amani, unaeka mazingira yale yale ya mwaka 2013 na 2016," amesema Allan akiongezea kwamba "mkataba unapovunjika, unavunjika vibaya sana".
Mikataba ya amani umesainiwa katika siku za hivi karibuni lakini imevunjika ndani ya masaa machache baada ya kusainiwa.
Jumuiya ya Kimataifa
Uvumilivu wa jumuiya ya kimataifa umekuwa ukitoweka, Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa likiiwekea Sudan Kusini vikwazo vya silaha.
Mnamo mwezi July, bunge la Sudan Kusini liliongeza muda wa serikali hadi mwaka 2021, hatua ambayo iliwakasirisha wanasiasa wa upinzani waliosema kwamba serikali ilikuwa katika mchezo kwenye meza ya mazungumzo ya kuleta amani ya kudumu.
Raia wa Sudan Kusini
Raia wa Sudan Kusini wanasema kwamba wamechoka na maisha ya vita na wanataka hali ya utulivu.
"Kwa kweli tunataka amani kwa sababu tumechoka na vita" amesema Santino Deng, mkaazi wa mji wa Juba.
Hata hivyo baadhi ya makundi ya kutetea haki za kibinadamu yamesifia mkataba wa amani uliofiikiwa hivi sasa, lakini yakaonya kwamba ni hatua ya mwanzo tu.
" Ili kuzuia vita kuzuka tena, mkataba huo unastahili kuhakikisha kwamba mamlaka mengi hayasalii katika mikono ya watu wachache," amesema Brian Adeba, naibu wa mkurugenzi wa shirika la sera - enough project- lenye makao makuu jijini Washington.