Jumapili, 7 Agosti 2016

HASARA ZA KUJIPENDEKEZA.


1. Hauwezi kumkemea huyo unayejipendekeza kwake hata kama anakosea.
2. Unakuwa Mtumwa kwa huyo unayejipendekeza kwake.
3. Unaifanya akili yako ishindwe kuzalisha  matunda maana Unakuwa Tegemezi kwa huyo unayejipendekeza kwake.
4. Utajikuta unakosana NA watu hasa wakimkosoa huyo unayejipendekeza kwake. Maana huntokubali akosolewe mbele yako.
5.Inakufanya kuwa mnafiki  ,Maana hata wewe kwenye uvungu wa moyo wako kuna vitu unaviona havipo sawa lakini  "UNAMEZEA TU " Kulinda kufukuzwa.
6. Inakuharibu kisaikolojia ,hasa pale ambapo  Hautapata kile Ulichokitegemea kwa Huyo unayejipendekeza kwake.
7.Inakufanya Uyanyonge MAONO uliyonayo kwa mikono yako mwenyewe, maana Muda mwingi unatafuta Jinsi ya kumpendeza  Huyo unayejipendekeza kwake. Badala ya kuwekeza Muda wako kwenye MAONO  Binafsi.
8.Kunakufanya Huyo  Unayejipendekeza kwake  awe
  "MUNGU MTU " ,Hivyo unajikuta unamsujudia kwa kila jambo.
9. Hauwezi kufanya MAAMUZI Binafsi  ni hadi huyo unayejipendekeza kwake akuamilulie, akikataa ndiyo basi tena.
10.Utagombana NA watu mara kwa mara, maana kila atakayejionyesha kuwa karibu  NA  huyo unayejipendekeza kwake, Utampiga mawe maana unafikiri, anaichukua nafasi yako.
11. Inakufanya uthamani wako Ushuke kabisa NA kudharaulika , Maana unaishi kwa kumtegemea Mwanadamu mwenzako bila yeye haukai mjini.
12. mungu wako anakuwa ni huyo UNAYEJIPENDEKEZA KWAKE.
13.Hauwi Mwanaume halisi /Mwanamke halisi, Maana walio Halisi wanayo misimamao Binafsi wala hawayumbishi  kama uliyo wewe kwa huyo, UNAYEJIPENDEKEZA KWAKE Maana umekuwa  ."BENDERA FUATA UPEPO "

USHAURI WA BURE
1.Acha Kujipendekeza.
2. Wewe ambaye MTU/WATU  WanajipendekeA kwako. ...kwa kuwa sasa unaabudiwa  (kimungu mtu wewe ),Mungu atakushusha hadi kuzimu.
3.HERI KUJIPENDEKEZA KWA MUNGU MAANA ANAKUWA NI MUNGU WAKO NA UNAKUWA MTUMWA WAKE NA ATAKUAMULIA MAAMUZI YAKO.

0 comments: