Kila mtu anapenda kuwa na maisha ya furaha, na ili kupata furaha hii tumekuwa tukikazana kufanya mambo mbalimbali.
Kwa bahati mbaya sana mengi ya mambo tunayofanya tukitarajia kupata furaha, yamekuwa hayatuletei furaha ya kudumu, badala yake yanatuletea raha za muda mfupi ila ukweli unabaki pale pale kwamba hatuna furaha.
Tulishajifunza kwenye moja ya makala kwamba furaha ya kweli inaanzia ndani yetu sisi wenyewe. Inaanzia pale ambapo tunajijua sisi wenyewe, tunajua ni nini hasa tunataka na jinsi gani tunaweza kufikia tunachotaka.
Pamoja na furaha kuanzia ndani yetu sisi wenyewe, kuna kitu kingine ambacho kinaanzia ndani yetu ambacho kinatuzuia kuwa na